ELIMU KWANZA

ELIMU KWANZA
KWETU FEDHA SIO KIPAUMBELE.

Friday 8 November 2013

Makosa 10 wanawake huyafanya wakiwa faragha-9

Tunaendelea na mada yetu ya Makosa 10 wanawake huyafanya wakiwa faragha kutoka pale tulipoiishia wiki iliyopita.
Endelea...
Nilishaeleza huko nyuma kwamba ni vizuri kuzungumza wakati wa tendo. Hata kama wewe ni mvivu, jibidishe katika kuulainisha ulimi wako ili uwe unatamka maneno matamu, yanayoongeza hamu na mzuka wa kuendelea kuwajibika shughulini.

Unaweza kudhani ni kitu kidogo lakini ukweli ni kwamba wengi wamepata alama nyingi na kuonekana bora zaidi kwa sababu ya maneno yao faragha, matamshi na ubunifu wa kusifia. Kitaalamu, maneno matamu hunogesha tendo kwa kuongeza mshawasha.
Dunia imechafuka, usaliti umekuwa mkubwa na watu hawaogopi. Tafakari; unasalitiwa na mwenzi wako ambaye anatenda dhambi kwa kutoka na mkali wa maneno yenye kutia ‘wazimu’ kunako eneo mahsusi. Akirudi kwako, anabaini wewe upoupo tu, kazi yako kuhema kwa nguvu na kufumba macho.

Anakosa msisimko, zaidi unamkata stimu kwa sababu kwa yule anayekusaliti hukutana na manjonjo mengi. Mwisho unajikuta unapigwa kibuti bila kupenda. Tafadhali sana, yapo mambo ambayo unaweza kusema huwezi na ukavumiliwa lakini siyo hili la kumfikisha mwenzi wako kwenye kilele cha ‘maraha’.

Narudia tena, usiseme mwenzi wako anatosheka kwa sababu anakwambia amefika kileleni, la hasha! Kitu ambacho unatakiwa kuzingatia kila siku ni kama raha unazompa zina kiwango stahiki. Hakikisha huoneshi udhaifu kwenye kipengele chochote.
Mpaka hapo, bila shaka tumekubaliana kuzungumza ni muhimu, jukumu ulilonalo ni kuangalia aina ya mazungumzo. Yale ambayo hayachombezi, hayana mshawasha, hayahusu tendo, maana yake hayana mashika katika kipengele ambacho wewe nay eye mpo.

Haiwezekani katikati ya tendo unaongea: “Jana ulichelewa kurudi nyumbani.” Kuzungumza hivyo ni kujikosea wewe mwenyewe, kwani utamfanya mwenzi wako akatike stimu, kwa hiyo hata kiwango chake cha uwajibikaji kitapungua, hivyo hatakuhudumia kwa kiwango bora.

Nyongeza hapa ni kujiepusha na makelele. JJifunze kunong’ona, tena unong’onaji wenyewe ufanye masikioni mwake. Pata picha umemkumbatia mwenzi wako, hisia zake zipo juu na mshawasha (orgasm), unasomeka kwa asilimia 100, halafu wewe unamnong’oneza maneno matamu.

Kufanya hivyo, utamfanya mwenzio achanganyikiwe. Kama hujui, huo ndiyo uchawi ambao unaweza kumsababishia mpenzi wako awe anakuwaza kila anapokuwa mbali na wewe. Picha yako itamjia kichwani mwake kwa utamu, kila atakapokuwa anafikiria tendo.
Sasa basi, kuhusu kuzungumza na kutozungumza, nakushauri ujibiidishe kuzungumza kwa kunong’ona. Lainisha ulimi ili sauti yako iwe inatoka ikiwa imejaa mahaba. Nong’ona sikioni kwake, hapo ndipo utapatia. Hili siyo jukumu la kihisia, mwanaume na mwanamke, wote ni wajibu wao.

DHIBITI MAYOWE
Miguno ya mahaba na zile sauti tamu za malalamiko, zinaruhusiwa. Mayowe ambayo yanaleta kelele kwa kawaida hayaruhusiwi. Unashauriwa kuyadhibiti ili usigeuke kero kwa mwenzi wako, ukamnyima uhuru wa kufurahia tendo, kadhalika naye aweze kukuhudumia inavyotakiwa.
Busara hapa ni kwamba kwa nyumba zetu za Uswahilini, huwezi kupiga mayowe halafu ukakwepa kusikika nje. Hivyo basi, mayowe yako yanaweza kumfanya mwenzi wako ashindwe kujiamini, aamue kupunguza dozi ili kukufanya usiendelee kupiga makelele.
Atakapopunguza, itakufanya ukose uhondo uliostahili kutoka kwake. Vilevile hali hiyo, itamfanya mwenzi wako kupoteza umakini wa tendo, kwani badala ya kwenda nawe sawa, mkipanda na kushuka, anaweza kukutegea na kusikilizia zaidi makelele yako.
Msimamo wako ni mmoja tu, kuacha makelele! Kama kuna kungwi alikufundisha uwe ‘unabweka’ hovyo, kwamba ndiyo utamkosha roho mwenzi wako, huyo naye hajui. Badili mtazamo, fuata mwongozo huu ili ukuweke kisasa, vilevile ukujenge kimahaba zaidi.

HITIMISHO
Pitia vipengele 10 ambavyo nimevibainisha katika makala haya, vifanyie kazi, nakuhakikishia kwamba utakuwa mpya kimahaba, mwenye mtazamo wa kisasa. Wewe ni bora sana, ni suala la kujibiidisha tu na utaona matunda yake.

No comments:

Post a Comment